Katika hali ilyowashtua wengi leo hapa Mbeya ni mwenyekiti wa CHADEMA kukihama chama hicho na kujiunga na chama kipya cha ACT.
Tukio hili limetokea leo eneo la Nanenane jijini Mbeya, ni habari za
kweli kabisa nimeshuhudia kwa macho yangu sijahadidhiwa,picha nitaweka
baadaye kidogo.
Ni mwenyekiti wa wilaya ya Mbeya vijijini jina lake anaitwa ELIA KIOLILE
na alitamka machache juu ya chama chake cha zamani kuwa demokrasia
ndani CHADEMA ni finyu na inatamkwa kwa maneno tu na si kwa vitendo.
Pia akizungumzia vikosi vya chama hicho vya redbriged kuwa
vinajuhusisha na vitendo vya vitisho na mambo ya hatari kama kupiga watu
na akasema hataki kuwa sehemu ya dhambi hizo na ndiyo maana ameamua
kujiondoa licha ya nafasi aliyonayo ya uenyekiti wa chama wilaya nafasi
ambayo alishinda kwenye uchaguzi wa majuzi kwa kupata asilimia 70% ya
kura na kutangazwa mshindi.
Pamoja naye, wamehamia pia mtunza hazina wa wilaya Mbeya vijiji na
mjumbe wa serikali ya mtaa kwa ticketi ya CHADEMA kata ya Nsalala mtaa
wa Zambia road Mbalizi.
0 comments:
Post a Comment